Notice: Function _load_textdomain_just_in_time was called incorrectly. Translation loading for the post-views-counter domain was triggered too early. This is usually an indicator for some code in the plugin or theme running too early. Translations should be loaded at the init action or later. Please see Debugging in WordPress for more information. (This message was added in version 6.7.0.) in /www/wwwroot/net.wazaelimu.com/wp-includes/functions.php on line 6131
Barua ya Kuteuliwa Kuwa Mwalimu wa Fedha (Mhasibu) wa Shule

Barua ya Kuteuliwa Kuwa Mwalimu wa Fedha (Mhasibu) wa Shule

SHULE YA MSINGI S.L.P ……,
……………………….
TAREHE :…………………….
MWL. _________________________________
SHULE YA MSINGI

YAH:- KUTEULIWA KUWA MWALIMU WA FEDHA (MHASIBU) WA SHULE.

Husika na kichwa cha habari hapo juu, kufuatia taratibu na kanuni za kazi katika utumishi wa Umma zinavyoelekeza. Kwa mamlaka niliyonayo kama Mwalimu mkuu Napenda kukutaarifu kuwa nimekuteua kushika nafasi tajwa hapo juu hadi hapo nitakapoamua kukubadilisha katika nafasi hiyo.

Kama mhasibu wa shule majukumu yafuatayo unapaswa kuyatekeleza:

i. Kuandaa vocha.

ii. Kuandaa hundi.

iii. Kuandaa taarifa ya mapato na matumizi.

iv. Kuandaa masuluhisho ya kibenki ( Bank reconciliation ).

v. Kuandaa taarifa ya robo mwaka.

vi. Kulipa posho mbalimbali za walimu.

vii. Kufanya kazi mbalimbali utakazopangiwa na mwalimu mkuu.

viii.Kumshauri mwalimu mkuu kuhusu mambo yote yahusuyo fedha.

Ikitokea changamoto yeyote katika kutekeleza majukumu hayo tafadhali shirikisha Uongozi wa shule pale inapobidi kufanya hivyo.

Nakutakia utekelezaji mwema na wenye mafanikio.

Wako katika utumishi.
………………………………

Leave a Comment