Notice: Function _load_textdomain_just_in_time was called incorrectly. Translation loading for the post-views-counter domain was triggered too early. This is usually an indicator for some code in the plugin or theme running too early. Translations should be loaded at the init action or later. Please see Debugging in WordPress for more information. (This message was added in version 6.7.0.) in /www/wwwroot/net.wazaelimu.com/wp-includes/functions.php on line 6131
Aina za Leseni/Madaraja Ya Leseni Za Udereva

Aina za Leseni/Madaraja Ya Leseni Za Udereva

Mahitaji ya Kupata Leseni ya Udereva kwa Mara ya Kwanza

Ili kupata leseni ya udereva kwa mara ya kwanza, unahitaji kutimiza mahitaji yafuatayo:

  1. Umri: Kuwa na umri wa miaka 18 au zaidi kwa magari na miaka 16 au zaidi kwa pikipiki.
  2. Mafunzo: Hudhuria mafunzo katika chuo kinachotambuliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na upate cheti cha kuhitimu.
  3. Leseni ya Kujifunza: Pata leseni ya kujifunza (provisional) kutoka TRA.
  4. Mtihani wa Nadharia: Fanya na ufaulu mtihani wa nadharia kuhusu sheria za barabarani na usalama.
  5. Mtihani wa Vitendo: Fanya na ufaulu mtihani wa vitendo wa kuendesha gari.
  6. Cheti cha Afya: Pata cheti cha afya kutoka kwa daktari kinachothibitisha kuwa una afya nzuri ya kuendesha gari.
  7. Malipo: Lipa ada zote zinazohitajika kwa TRA.

 Majaraja ya leseni za udereva

Tanzania ina madaraja mbalimbali ya leseni za udereva, kulingana na aina ya gari unayotaka kuendesha:

  • Daraja A: Pikipiki (za ukubwa tofauti)
  • Daraja B: Magari ya binafsi
  • Daraja C: Magari ya abiria (daladala, mabasi)
  • Daraja D: Magari ya mizigo
  • Daraja E: Magari yote (isipokuwa ya abiria na pikipiki)
  • Daraja F: Mitambo maalum (forklifts, graders)
  • Daraja G: Mitambo ya kilimo na migodi (tractors)
  • Daraja H: Leseni ya kujifunza (provisional)

Leave a Comment