Notice: Function _load_textdomain_just_in_time was called incorrectly. Translation loading for the post-views-counter domain was triggered too early. This is usually an indicator for some code in the plugin or theme running too early. Translations should be loaded at the init action or later. Please see Debugging in WordPress for more information. (This message was added in version 6.7.0.) in /www/wwwroot/net.wazaelimu.com/wp-includes/functions.php on line 6131
Barua ya Kuteuliwa Kuwa Mwalimu wa Afya na Mazingira wa Shule

Barua ya Kuteuliwa Kuwa Mwalimu wa Afya na Mazingira wa Shule

SHULE YA MSINGI S.L.P …………,

TAREHE ………………..

MWL :_____________________________

SHULE YA MSINGI

YAH:- KUTEULIWA KUWA MWALIMU WA AFYA NA MAZINGIRA.

Husika na kichwa cha habari hapo juu, kufuatia taratibu na kanuni za kazi katika utumishi wa Umma zinavyoelekeza. Kwa mamlaka niliyonayo kama Mwalimu mkuu, napenda kukutaarifu kuwa nimekuteuwa kushika nafasi tajwa hapo juu hadi hapo nitakapoamua kukubadilisha katika nafasi hiyo. Kama mwalimu wa mazingira una wajibu wa kutekeleza yafuatayo:

i.kuhamasisha na kufuatilia utunzaji wa mazingira shuleni.

ii.kusimamia ukarabati wa samani mbalimbali za shule.

iii.kuhakikisha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji ni salama na rafiki shuleni.

iv.kuhakikisha shule inapangwa mawe na kupakwa chokaa.

v.kuhamasisha wanafunzi upandaji wa maua na miti shuleni.

vi.kuhakikisha mazingira ya shule ni safi na yanavutia.

vii.kufanya kazi zingine zote utakazopangiwa na mwalimu mkuu.

viii.kumshauri mwalimu mkuu kuhusu mambo yote yahusuyo mazingira ya shule.

Ikitokea changamoto yeyote katika kutekeleza majukumu hayo tafadhali shirikisha Uongozi wa shule pale inapobidi kufanya hivyo.

Nakutakia utekelezaji mwema na wenye mafanikio.

Wako katika utumishi.
………………………………

Leave a Comment