Notice: Function _load_textdomain_just_in_time was called incorrectly. Translation loading for the post-views-counter domain was triggered too early. This is usually an indicator for some code in the plugin or theme running too early. Translations should be loaded at the init action or later. Please see Debugging in WordPress for more information. (This message was added in version 6.7.0.) in /www/wwwroot/net.wazaelimu.com/wp-includes/functions.php on line 6131
Barua ya Uteuzi Mwalimu wa Miradi (EK) wa Shule

Barua ya Uteuzi Mwalimu wa Miradi (EK) wa Shule

SHULE YA MSINGI S.L.P …..,
TAREHE :………………….
MWL :_____________________
SHULE YA MSINGI .

YAH:- KUTEULIWA KUWA MWALIMU WA MIRADI (EK) WA SHULE

Husika na kichwa cha habari hapo juu, kufuatia taratibu na kanuni za kazi katika utumishi wa Umma zinavyoelekeza. Kwa mamlaka niliyonayo kama Mwalimu mkuu Napenda kukutaarifu kuwa nimekuteuwa kushika nafasi tajwa hapo juu hadi hapo nitakapoamua kukubadilisha katika nafasi hiyo.

Kama mwalimu wa miradi unapaswa kutekeleza majukumu yafuatayo:

i.kupanga na kuratibu shughuli zote zinazohusiana na miradi ya shule.

ii.kuhakikisha shule ina eneo la kutosha kwa ajili ya kilimo.

iii.kuandaa mapato na matumizi ya miradi yote ya shule.

iv.kuhamasisha kilimo cha kisasa shuleni.

v.kufanya kazi zingine zote utakazopangiwa na mwalimu mkuu.

vi.kumshauri mwalimu mkuu kuhusu mambo yote yahusuyo miradi ya shule.

Ikitokea changamoto yeyote katika kutekeleza majukumu hayo tafadhali shirikisha Uongozi wa shule pale inapobidi kufanya hivyo.

Nakutakia utekelezaji mwema na wenye mafanikio.

Wako katika utumishi.

………………………………

Leave a Comment