Notice: Function _load_textdomain_just_in_time was called incorrectly. Translation loading for the post-views-counter domain was triggered too early. This is usually an indicator for some code in the plugin or theme running too early. Translations should be loaded at the init action or later. Please see Debugging in WordPress for more information. (This message was added in version 6.7.0.) in /www/wwwroot/net.wazaelimu.com/wp-includes/functions.php on line 6131
Jinsi Ya Jinsi ya Kununua Tiketi za Mpira Airtel Money

Jinsi Ya Jinsi ya Kununua Tiketi za Mpira Airtel Money

Zifuatazo ni hatua za Kununua Tiketi za Mpira kwa Airtel Money

Piga *150*60#

Anza kwa kupiga *150*60# kwenye simu yako. Hii itakupeleka moja kwa moja kwenye menyu ya Airtel Money.

Chagua 5 > Lipa Bill

Baada ya kuingia kwenye menyu ya Airtel Money, chagua namba 5 ambayo ni “Lipa Bill”.

Chagua # > Next

Chagua # ili kuendelea na hatua inayofuata.

Chagua 8 > Malipo Mtandao

Kwenye menyu inayofuata, chagua namba 8 ambayo ni “Malipo Mtandao”.

Chagua 1 > Tiketi za Michezo

Chagua namba 1 kwenye menyu ya “Tiketi za Michezo”.

Chagua 1 > Football Tickets

Baada ya hapo, chagua namba 1 kwa “Football Tickets”.

Chagua Mechi Unayotaka Kulipia

Kwenye orodha ya mechi zinazopatikana, chagua mechi unayotaka kulipia tiketi.

Chagua Aina ya Tiketi Unayotaka Kulipia

Baada ya kuchagua mechi, utaulizwa uchague aina ya tiketi unayotaka kulipia.

Weka Namba ya Kadi yako ya (N-Card)

Weka namba ya kadi yako ya N-Card ili kukamilisha mchakato wa malipo.

Ingiza Namba ya Siri

Ingiza namba yako ya siri ya Airtel Money ili kuthibitisha malipo.

Thibitisha

Hatua ya mwisho ni kuthibitisha malipo yako. Utapokea ujumbe wa kuthibitisha kuwa malipo yako yamekamilika na tiketi yako imekatwa.

Leave a Comment