Notice: Function _load_textdomain_just_in_time was called incorrectly. Translation loading for the post-views-counter domain was triggered too early. This is usually an indicator for some code in the plugin or theme running too early. Translations should be loaded at the init action or later. Please see Debugging in WordPress for more information. (This message was added in version 6.7.0.) in /www/wwwroot/net.wazaelimu.com/wp-includes/functions.php on line 6131
Jinsi ya Kubadili Jina Kwenye Cheti cha NECTA PSLE, CSEE & ACSEE

Jinsi ya Kubadili Jina Kwenye Cheti cha NECTA PSLE, CSEE & ACSEE

Ninabadilishaje jina kwenye cheti? Ninabadilishaje jina kwenye cheti chaa form four? Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) hushughulikia maombi ya marekebisho ya majina ya watahiniwa yaliyokosewa kuandikwa katika mitihani ya Shule za Msingi, Sekondari na Vyuo vya Ualimu. Ufuatao ni utaratibu unaotumika katika kuwasilisha maombi na kufanya marekebisho.

MASHARTI YA MAREKEBISHO YA MAJINA

Maombi ya marekebisho yawasilishwe katika kipindi kisichozidi mwaka mmoja baada ya matokeo ya mtihani kutolewa.

Marekebisho ya jina ni lazima yawe na lengo la kufanya jina linalohitajika lifanane na jina lililotumika katika mtihani wa sifa (awali).

Marekebisho yanayokusudia kuongeza jina jipya au kuondoa/kubadilisha jina (Mfano: Magina kuwa

Madoba) hayaruhusiwi.

  1. Marekebisho yanayolenga kuboresha herufi zisizoathiri Matamshi ya jina linapotamkwa yanaweza kuombwa kufanyika.
  2. Msingi pekee wa marekebisho ya jina ni mtihani wa sifa (awali) na sio jina lililopo katika viapo vya mahakama, vyeti vya ndoa, ubatizo n.k.
  3. Cheti halisi chenye jina lilikosewa ni lazima kirudishwe NECTA kwa ajili ya mchakato wa marekebisho.

HATUA ZA KUFUATA WAKATI WA KUFANYA MAOMBI

1. Fungua tovuti (Website) ya NECTA (www.necta.go.tz)

2. Chagua na ubonyeze huduma mtandao (E-services), halafu chagua (Replacement Certificate)

3. Bonyeza “Generate Control Number” ili kupata nambari ya malipo (Control Number)

4. Ingiza taarifa zako kama hapa chini ili kupata: Control Number”

5. Bonyeza “save” baada ya kujaza taarifa zako kwa usahihi.

6. Lipia ada ya marekebisho ya jina ya Tsh.35, 000/= (kwa cheti kimoja) kupitia benki au mitandao ya simu kwa kutumia ‘Control number’ uliyotengeneza.

Baada ya kufanya malipo

7. Bonyeza Marekebisho ya Majina (Correction of Names) na ufanye maombi (Apply/New)

8. Ingiza nambari ya simu ya mkononi na nambari ya malipo (Control Number).

9. Jaza fomu ya maombi mtandao (Online Application Form) kisha Wasilisha ombi kwa kubofya ‘Submit’.

MAJIBU

Baada ya marekebisho kufanyika, Hati ya Matokeo (Results Slip) au cheti kipya chenye marekebisho kitatumwa kwa mkuu wa shule au kwa mtahiniwa (endapo si mwanafunzi).

Mawasiliano

Eneo la Viwanda Mikocheni, Barabara ya Bagamoyo,

S.L.P. 2624 au 32019 DAR-ES-SALAAM TANZANIA

Simu: +255-22 2700493-6/9 +255-22-2772423

Nukushi: +255-22-2775966

Barua pepe: esnecta@necta.go.tz,

Tovuti: www.necta.go.tz

Leave a Comment