Huu Apa Muongozo wa Jinsi ya Kupata Cheti cha Kuzaliwa Kwa Mtu Mzima
- Jaza Fomu ya Usajili wa Kizazi, B3 (ipatikane kwenye ofisi za RITA au mtandaoni).
- Ambatanisha picha ya mtoto (passport size) na nyaraka zinazohitajika (kadi ya kliniki, cheti cha ubatizo, barua kutoka serikali za mitaa, vyeti vya shule, n.k.).
- Kwa wale waliozaliwa zamani sana, utahitaji pia kadi ya taifa, kadi ya kupigia kura, au bima ya afya.
- Lipa ada ya shilingi 20,000.
Nyaraka za Ushahidi: Mzazi au mlezi anatakiwa kuwasilisha nyaraka mbalimbali kama vile:
- Kadi ya kliniki ya mtoto
- Cheti cha ubatizo (ikiwa kipo)
- Barua kutoka mamlaka za serikali (mfano, ofisi ya mtendaji wa kata/kijiji)
- Cheti cha kumaliza elimu ya msingi au sekondari
Nyaraka za Utambulisho (kwa waliozaliwa zamani): Kwa wale waliozaliwa miaka mingi iliyopita, wanatakiwa kuambatanisha nyaraka za ziada kama vile:
- Kadi ya Utaifa pamoja na Kadi ya Kura au Bima ya Afya.
- Leseni ya Gari (lazima iambatane na Kadi ya Utaifa au Kadi ya Kura).
Kwa Nini Cheti cha Kuzaliwa ni Muhimu?
Cheti cha kuzaliwa ni kitambulisho muhimu sana kinachothibitisha utambulisho wako, tarehe ya kuzaliwa, na uraia wako. Unahitaji cheti hiki kwa mambo mengi muhimu maishani, kama vile:
- Kupata hati ya kusafiria (pasipoti)
- Kuandikishwa kupiga kura
- Kuomba ajira
- Kuomba mikopo
- Kufungua akaunti ya benki
- Kusajili ndoa
Leave a Comment