Notice: Function _load_textdomain_just_in_time was called incorrectly. Translation loading for the post-views-counter domain was triggered too early. This is usually an indicator for some code in the plugin or theme running too early. Translations should be loaded at the init action or later. Please see Debugging in WordPress for more information. (This message was added in version 6.7.0.) in /www/wwwroot/net.wazaelimu.com/wp-includes/functions.php on line 6131
Matokeo ya Mitihani ya Taifa ya Ufundi Stadi VETA NACTVET Kwa Msimu wa Desemba 2024 - Waza Elimu

Matokeo ya Mitihani ya Taifa ya Ufundi Stadi VETA NACTVET Kwa Msimu wa Desemba 2024

MATOKEO YA MITIHANI YA TAIFA YA UFUNDI STADI KWA MSIMU WA DESEMBA, 2024

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) linapenda kuufahamisha umma kuwa limeidhinisha matokeo ya Mitihani ya Taifa ya Ufundi Stadi katika ngazi ya I, II na III iliyofanyika mwezi Desemba, 2024. Mitihani hiyo iliratibiwa na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA).

Jumla ya watahiniwa 41,331 walifanya mitihani ya Taifa ya Ufundi Stadi ambapo wasichana ni 14,215 sawa na asilimia 34.4 na wavulana 27,116 sawa na asilimia 65.6.

Matokeo ya Mitihani

Kati ya watahiniwa 41,331 waliofanya mitihani, watahiniwa 35,355 sawa na asilimia 86 wamefaulu. Watahiniwa 5,976 sawa na asilimia 14 wanapaswa kurudia mitihani yao.

Matokeo ya mitihani hiyo ni katika fani za Ufundi Magari, Ufundi Umeme, Ushonaji, Uchapaji, Usindikaji Vyakula, Huduma za Biashara, Kilimo, Madini, Ukarimu na Utalii pamoja na Urembo.

Kufutiwa matokeo

Watahiniwa wawili (2) wamefutiwa matokeo yao kutokana na ukiukwaji wa taratibu za mitihani.

Kupata matokeo ya mitihani ya CBA, Uanagenzi na NABE kwa msimu wa Desemba, 2024 bonyeza hapa Chini

TAARIFA YA MATOKEO YA MITIHANI YA UFUNDI STADI MSIMU WA DESEMBA 2024

Kwa ufafanuzi zaidi tafadhali wasiliana nasi kupitia barua pepe: dac@veta.go.tz na namba ya simu 0755267489

Leave a Comment