Notice: Function _load_textdomain_just_in_time was called incorrectly. Translation loading for the post-views-counter domain was triggered too early. This is usually an indicator for some code in the plugin or theme running too early. Translations should be loaded at the init action or later. Please see Debugging in WordPress for more information. (This message was added in version 6.7.0.) in /www/wwwroot/net.wazaelimu.com/wp-includes/functions.php on line 6131
Mwalimu Daraja la IIIA Maaana Yake Nini?

Mwalimu Daraja la IIIA Maaana Yake Nini?

Mwalimu Daraja la IIIA huyu ni mwalimu mwenye Astashahada (Cheti) ya Ualimu.

Sifa Kuu

Cheti cha Mtihani wa Taifa wa Kidato cha nne na kufaulu mafunzo ya Ualimu ya miaka miwili (2) kutoka Vyuo vya Ualimu vinavyotambulika na Serikali na kutunukiwa cheti cha Ualimu Daraja la IIIA.

MAJUKUMU YA KAZI

i. Kuandaa azimio la kazi, maandalio ya masomo, nukuu za masomo na Mpango wa Kazi wa majukumu mengine aliyokabidhiwa;

ii. Kutengeneza na Kufaraghua zana za kufundishia na kujifunzia;

iii. Kufundisha, kufanya Tathimini na kutunza kumbukumbu za Maendeleo ya Wanafunzi;

iv. Kusimamia na kufuatilia mahudhurio ya wanafunzi Shuleni na Darasani;

v. Kusimamia malezi ya wanafunzi Kiakili, Kimwili, Kiroho na kutoa ushauri nasaha na unasihi;

vi. Kutoa ushauri wa kitaalamu na kitaaluma kuhusu maendeleo ya Elimu;

vii. Kusimamia na utunzaji wa vifaa na mali za shule; na

viii. Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Shule kulingana na majukumu ya Shule.

Msharahara

Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali anaanzia TGTS- B

Leave a Comment