Notice: Function _load_textdomain_just_in_time was called incorrectly. Translation loading for the post-views-counter domain was triggered too early. This is usually an indicator for some code in the plugin or theme running too early. Translations should be loaded at the init action or later. Please see Debugging in WordPress for more information. (This message was added in version 6.7.0.) in /www/wwwroot/net.wazaelimu.com/wp-includes/functions.php on line 6131
NIDA Kusitisha Matumizi ya Namba za NIDA Kwa Waliotumiwa SMS Kwenda Kuchukua Vitambulisho Vyao

NIDA Kusitisha Matumizi ya Namba za NIDA Kwa Waliotumiwa SMS Kwenda Kuchukua Vitambulisho Vyao

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa, NIDA inatarajia kusitisha matumizi ya namba za vitambulisho vya NIDA kunanzia Mei 1, mwaka huu, kwa wananchi wote waliotumiwa ujumbe mfupi (SMS), kwenda kuchukua vitambulisho vyao na hawajafanya hivyo.

Akizungumza mapema leo ofisini kwake, Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, James Kaji amesema NIDA imesikitishwa na idadi ndogo ya wananchi wanaojitokeza kuchukua vitambulisho vyao.

“Inasikitisha sana, tumekuwa tukituma ujumbe mfupi kwa wananchi kuwaelekeza ni mahali gani waende kuchukua vitambulisho vyao lakini idadi ni ndogo sana.

“NIDA tumeamua kuwa tutasitisha matumizi ya namba za vitambulisho, kwa wale wote ambao wameshatukiwa vitambulisho lakini hawajachukua,” amesema Kaji.

Katika hatua nyingine, Kaji amesema NIDA ipo katika hatua za mwisho katika kuja na mfumo mpya wa kusajili kuanzia watoto wadogo.

Leave a Comment